Saturday, September 10, 2016

Skuvi ltd promo fliers

Friday, June 10, 2016

Muonekano wa biashara yako na matokeo yake.

Muonekano wa biashara yako na matokeo yake.

Hali ya mzunguko na mfumo wa biashara imebadilika sana hapa nchini na hii imechangiwa na kuongezeka kwa makampuni ya kigeni ambayo yamekuwa yakiongeza chachu ya kuendelea kufanya zaidi ya pale wazawa wanapofanya, na tofauti kubwa ambayo inafanya kampuni nyingi na biashara nyingi za nje kufanikiwa ni Branding, asilimia kubwa ya hizo kampuni huingia nchini tayari zikiwa zimeshajibrand hivyo inakuwa rahisi kupata nafasi katika soko la ndani.

Kinyume cha hapo asilimia kubwa ya biashara au kampuni zetu wazawa hazijafanya Branding ambayo ndio uti wa mgongo wa biashara, matokeo yake imekuwa hatuwezi kuuza ndani sababu hazina muonekano mzuri na hatuwezi kuuza nje sababu pia hazijafanyiwa branding nzuri.

Baada ya serikali kuiona changamoto hiyo ikaanza kusisitiza wafanyabiashara kufanya branding vizuri( kuboresha  utengenezaji na upakiaji wa bidhaa uwe mzuri na wa kuvutia ili bidhaa zetu zipate nafasi hata katika soko la nje kwa wingi).

Hivyo mabadiliko hayo yameathiri pia na soko la ndani, kwa vile tunaagiza vitu vingi kutoka nje, vile vinavyotengenezwa ndani vikiwa havijabrandiwa vinakosa soko katika eneo lake la ushindani, watu sasa wananunua brand sio bidhaa ukiwaaminisha bidhaa yako ni bora na akaikuta bidhaa yako ni bora basi utakuwa umempata huyo mteja, Je umejibrand vyema kiasi cha kupata nafasi katika eneo lako la ushindani? una nafasi katika soko lako?

Kama bado Karibu Legacy sasa tukubrand kulingana na biashara na eneo lako la ushindani, njoo tukutengenezee stika/lebo kwa ajili ya bidhaa zako ili ujitambulishe vyema,tukutengenezee utambulisho ( nembo) ambayo itakuwalisha kwenye kila bidhaa yako, tukutengenezee vipeperushi muda wa kuandika maelezo marefu ya bidhaa yako umekwisha iweke kwenye dizaini nzuri na watu wataisoma.Karibu sasa ufanye kazi  na watu wanaotambua umuhimu wa biashara yako kwa mteja wako.

Karibu msimu huu wa Ramadhan kuna punguzo kubwa katika bidhaa zetu, maendeleo yako ndio kazi yetu.

Tunahusika na shughuli za Printing, Graphics design, Webtech na Stationeries.Mawasiliano 0713 603699.

Monday, June 6, 2016

Nembo yako inamaanisha nni?

Je wewe ni mfanya biashara au mjasiriamali au mfanyabiashara?umetengenezaje nembo yako? inakidhdi vigezo vya soko lako?

Kwanza Logo ni alama au nembo iliyodizainiwa mahsusi kwa ajili ya biashara yako, inayotumika kukutambulisha nje na ndani ya ofisi. Au Logo ni alama au nembo inayotumika kutambulisha huduma,bidhaa,kampuni au mfumo wowote wa vikundi.

Kwanini biashara yako inahitaji nembo
1.Humpa mteja maana au tafsiri ya biashara yako japo inaweza kuwa sio sawa na ya kwako
2.Huonyesha muonekano unaotakiwa
3.hukuongezea hadhi
4.huonyesha utofauti wako na wengine katika soko
5.Kuwa na muonekano wa kuvutia
6.Hujipanga yenyewe kwa malengo flani ya soko.

Vitu vya kuangalia unapotengeneza logo
1. Iwe ya kipekee
2. Inatakiwa iwasilishe uhalisia wa biashara ,bidhaa au huduma
3. Iwe na uwezo wa kuonekana kwa wateja unaowategemea
4. Iwe na uwezo wa kusimama na kujiimarisha muda hadi muda ( isipitwe na wakati)
5. Iwe na uwezo wa kutumika na kuoneka kwenye kila nyanja yamawasiliano.

Ushindani umeongezeka sana kwa sasa, sokoni bila ya kuwa na bidhaa iliyofanyiwa brand vizuri utalazimishwa kufuata wengine, hivyo hakikisha unafuata mtu au kampuni inayofahamu vizuri branding na( kudizaini ili wakutengenezee nembo itakayokidhi soko na matakwa yake.kwa mawasiliano zaidi 0713 603699 karibu tukutengenezee nembo bora kabisa kwa sasa tuna ofa 3 msimu huu wa Ramadhan.

Tengeneza nembo kwa Tshs.50,000 tu.

Print  business kwa Tshs. 20,000 Kwa piece 100.

Dizaini na kuprint flier/Vipeperushi. =120,000(Fliers 100)

Karibuni.

Tuesday, May 31, 2016

Je unatambua vitu vinavyotakiwa kuonekana kwenye lebo yako?

Je unatambua lebo au stika ya bidhaa yako inahitaji kuwa na vitu gani ili ikupe muonekano sahihi?

Tumepokea wajasiriamali wengi na wafanyabiashara wadogo wengi  wakihitaji huduma ya kutengenezewa lebo ama stika kwa ajili ya bidhaa zao, lakini tofauti na ambavyo inatakiwa kuwa asilimia kubwa huja wakiwa na mawazo tofauti kabisa na uhalisia halisi wa stika au lebo inavyotakiwa kuwa.
Lebo yako unayoitengeneza tambua inatakiwa iwe na maelezo ya mmiliki wa bidhaa au brand au brand husika kuwa ndio mmiliki wa brand.mfano wake ni kama ufuatao mmiliki wa soda za Fanta,Sprite na Cocacola ni Cocacola company. Hivyo katika soda za Fanta na Sprite ubavuni zimeandikwa “ a product of Cocacola company” (bidhaa ya kampuni ya cocacola ) lakini katika soda ya cocacola hakuna maandishi hayo ikimaanisha ndio bidhaa mama y azote…Lebo yako inatakiwa iwe na nembo mbili kama mmilika anabidhaa zaidi ya moja au moja kama mmiliki anabidhaa moja tu inayomtambulisha sokoni, hivyo usikimbilie kutengeneza stika ama lebo bila ya kuwa na nembo.
Kitu kingine ni nembo za uhalishaji kama Barcode,TBS na zingine hizi unatakiwa uzipate kutoka sehemu husika ambazo wanatoa ukija kudizaini unakuwa tayari umeshapewa ruhusa ya kuzitumia sio unaemfuata akudizainie ndio akuweke itakuwa kinyume na sheria na mkikamata litakuwa ni kosa la jinai.

Kitu kingine ni kujitahidi kuwa tofauti na wengine brand inatakiwa iwe tofauti hauwezi kupata nafasi katika soko kwa muonekano sawa na wenzako ila kwa kujitofautisha na wenzako, ndio maana makampuni ya simu yote yanatoa huduma zile zile lakini hayafananishi matangazo au ofa .

Karibu Legacy Impresion Company tukudizainie na kukutengenezea muonekano wa tofauti na sahihi katika soko lako la ushindani ili upate nafasi katika macho ya wateja wako…kwa sasa tunaofa nyingi kwa ajili ya msimu wa sabasaba kwa bidhaa zifuatazo Businesscards,Fliers ( Vipeperushi)Stika/Lebo,Nembo,Branding package na vingine vingi wasiliana nasi 0713603699 au info@legacytz.com.

Kuendelea kuona post na kazi zetu like na kushare page hii kwa ofa nyingi zaidi zinazoendelea kila siku www.facebook.com/legacy244